- 8,486 viewsDarzeni ya wanajeshi wa Congo wamewekwa kizuizini huko Bukavu, mji mkuu wa jimbo la Kivu Kusini, wakati mamlaka zikijiandaa kuwafungulia mashtaka wanajeshi wasiopungua 75 kwa kukimbia jeshini na vitendo vya ghasia dhidi ya raia, ikiwemo mauaji na uporaji. Kanda ya video kwenye mtandao wa kijamii iliyothibitishwa na Reuters Jumatatu (Februari 10) iliwaonyesha watu wakiwa na mavazi ya kiraia wakiingizwa kwenye Jela Kuu huko Bukavu. Mtazamaji katika kanda hiyo ya video aliwashutumu kuwa ni wanachama wa kikundi cha Cheetahs, kitengo cha jeshi la Congo, akisema “wanavuruga amani yetu.” Kuhusishwa kwa wafungwa katika video hiyo haukuweza kuthibitishwa na vyanzo huru. Reuters imethibitisha eneo hilo ni Bukavu kwa kulinganisha kuta za jela hiyo, lango kuu, miti yenye kuizunguka na milima na picha za satellite za eneo hilo. Wakati tarehe hasa ya kutolewa kanda hiyo ya video haikuweza kuthibitishwa na vyanzo huru, ilikuwa imepakuliwa kabla ya Jumatatu siku ya kesi. Chanzo cha jumuiya ya kiraia huko Kavumu, mji ulioko kilomita 35 kaskazini mwa Bukavu, ameiambia Reuters kuwa wanajeshi waliokimbia waliwauwa watu 10, wakiwemo saba kati yao waliokuwa wameketi baa Ijumaa jioni. Ofisi ya mwendesha mahtaka ya jeshi ilisema wanajeshi hao wanakabiliwa na mashtaka ya kukimbia kutoka mstari wa mbele baada ya waasi wa M23 kuuteka mji wa Nyabibwe, ulioko kilomita 70 kaskazini mwa Bukavu. Wanatuhumiwa pia kuhusika na ubakaji, mauaji, uporaji na uasi. (Reuters). #drc #congo #m23 #reels #voa
Wanaodaiwa kukimbia jeshini wawekwa jela kabla ya kesi kusikilizwa
- - 🔴 KTN LIVE STREAM ››
- 26 Jun 2025 - His remarks came amid nationwide protests held to mark one year since the deadly June 25, 2024, anti-government demonstrations.
- 26 Jun 2025 - Shabiki, through its Na Jamii corporate social responsibility initiative, proudly sponsored the KidsToKids Charity Golf Tournament, a one-of-a-kind event that raised funds to support education for underprivileged children in Kenya.
- 26 Jun 2025 - Some 26 Nyandarua County government vehicles were torched during Wednesday’s demonstrations to mark the first anniversary of last year’s anti-Finance Bill protests.
- - 16 deaths recorded in Wednesday protests: Amnesty Kenya
- 26 Jun 2025 - Iran's intelligence services have arrested 26 people, accusing them of collaborating with Israel, state media Fars news agency reported, days after a ceasefire between the two countries was announced.
- 26 Jun 2025 - Sixteen people died during nationwide anti-government protests in Kenya on Wednesday, most of them killed by police, the head of Amnesty Kenya said, a year after deadly demonstrations against a tax bill culminated in the storming of parliament.
- 26 Jun 2025 - Ecuador's president announced Wednesday that the country's most-wanted fugitive, Los Choneros gang leader "Fito," had been recaptured over a year after his escape from prison triggered a wave of violence.
- 26 Jun 2025 - This follows the conduct witnessed between police and protesters during the June 25 protests.
- 26 Jun 2025 - Busia Senator Okiya Omtatah has called on protesting youth to resist the temptation of storming the State House, urging them instead to focus their energy on achieving lasting change through democratic means. Speaking during an interview on a local TV…
- 26 Jun 2025 - Pastor Dorcas Rigathi has urged sustained prayers following the deadly Gen Z memorial protests that left at least eight people killed and 400 others injured across the 27 counties in Kenya where the demos took place. In a statement on Thursday, June 26…