- 199 viewsWaasi wa kikundi cha Hayat Tahrir al-Sham (HTS) wamesema walikuwa wameikamata miji ya Syria ya Talbis na Rastan. Hatua hiyo imewafikisha ndani ya kilometa kadhaa karibu na mji wa Homs, kanda za video katika mitandao ya kijamii Ijumaa (Desemba 6) zinaonyesha kile kilichosemwa ni waasi wakipita na magari katika mji wa Rastan. Kanda ya video hiyo iliyochukuliwa kutoka juu ya jengo moja, iliwaonyesha wapiganaji hao wakipita na magari na pikipiki wakifyatua risasi hewani kusherehekea wakati msafara huo ulipopita mjini humo. Shirika la Habari la Reuters liliweza kuthibitisha eneo hilo kuwa ni Rastan, mji ulioko takriban kilomita 20 kaskazini mwa Homs, kutokana na mpangilio wa mitaa, majengo, mnara wa msikiti na mnara wa saa unaonekana kutoka mbali unaofanana na picha za satalaiti na picha za kumbukumbu. Reuters haikuweza kuthibitisha tarehe maalum video hiyo ilichukuliwa, lakini Kikundi kinachofuatilia haki za binadamu Syria kimeripoti kuwa mji huo ulichukuliwa na waasi Ijumaa (Desemba 6). Mashambulizi ya mabomu yaliyofanywa na Russia usiku kucha yameharibu daraja la Rastan katika barabara kuu ya M5, ambayo ndiyo njia kuu kwenda Homs, kuwazuia waasi hao kulitumia kusonga mbele, afisa wa jeshi wa Syria ameiambia Reuters. Hezbollah imetuma idadi ndogo ya “vikosi vya uangalizi” kutoka Lebanon kwenda Syria usiku kucha kuwasaidia kuzuia waasi wanaipinga serikali kuukamata mji wa kimkakati wa Homs, maafisa wawili wa ngazi ya juu w wa Lebanon wameiambia Reuters. Afisa wa jeshi la Syria na maafisa wawili wa kanda ambao wako karibu na Tehran pia wameiambia Reuters kuwa vikosi maalum kutoka kikundi kinachoungwa mkono na Iran, Hezbollah walivuka kutoka Lebanon na kuingia Syria usiku kucha na wameanza ulinzi wa Homs. - Reuters #waasi #hayattahriralsham #syria #tablis #rastan #hezbollah #iran #voa #voaswahili
Waasi wa Hayat Tahrir al-Sham waiteka miji miwili chini ya serikali
- - UNFILTERED ››
- 26 Jun 2025 - In a statement released Thursday, the country's leading legal body expressed condolences to the families of the eight people confirmed to have died during the nationwide protests, one year after the 2024 anti-Finance Bill demonstrations.
- 26 Jun 2025 - The Kenya Union of Journalists (KUJ), Kenya Editors Guild (KEG), Association of Media Women in Kenya (AMWIK), and Kenya Correspondents Association have filed a petition in the High Court claiming that the government's actions violate several fundamental…
- 26 Jun 2025 - Speaking a day after the nationwide demonstrations, Kimilili MP Didmus Barasa criticized court-imposed restrictions on police use of force, claiming they left officers powerless in the face of unrest.
- 26 Jun 2025 - The incident occurred when two officers—one from the Directorate of Criminal Investigations (DCI) and the other from the general police service—were overcome by the weight of the mast, which collapsed and came into contact with live electricity cables…
- 26 Jun 2025 - President William Ruto has assented to the 2025 Finance Bill at State House, Nairobi after MPs passed the proposed legislation last week.
- 26 Jun 2025 - Aroko, who was previously arrested and treated as a suspect in the high-profile case, was freed after the Directorate of Criminal Investigations (DCI) reviewed the evidence and opted to enlist him as a key witness.
- 26 Jun 2025 - Action for Sustainable Change (AFOSC-Kenya) has condemned the violence reported in parts of the country during the June 25 anniversary demonstrations.
- 26 Jun 2025 - Property of unknown value was stolen and destroyed during the protests.
- 26 Jun 2025 - Four casualties from Wednesday’s June 25 anniversary demonstrations are still admitted at the Matuu Level IV hospital in Machakos County with gunshot wounds.
- 26 Jun 2025 - Most of these vehicles are often sold at auctions.