- 103 viewsMaelfu ya watu wamekusanyika katika miji mbalimbali kote Ugiriki Ijumaa kushinikiza haki ifanyike katika maadhimisho ya pili ya ajali mbaya ya treni kuwahi kutokea, huku wafanyakazi katika sekta ya usafiri wa ndege, majini na treni wakigoma. Watu 57 walifariki wakati treni ya abiria iliyokuwa imejaa wanafunzi ilipogongana na treni ya mizigo Februari 28, 2023, karibu na Tempi gorge huko katikati ya Ugiriki Miaka miwili baadaye, mianya ya usalama ambayo ilisababisha ajali hiyo haijatatuliwa, uchunguzi ulionyesha hivyo Alhamisi. Uchunguzi wa kujitegemea wa mahakama bado haujakamilika, na hakuna aliyehukumiwa katika ajali hiyo. Maandamano ya umma yalikuwa yamepangwa kufanyika katika darzeni ya miji kote nchini. Safari zote za ndege za ndani na za kimataifa zilisitishwa wakati waongoza ndege wakiungana na waendesha feri, treni, madaktari, mawakili na waalimu katika mgomo wa jumla wa saa 24 kuwaenzi waathirika wa ajali hiyo. Biashara zilifungwa na majumba ya burudani yalifuta maonyesho. Hadi kufikia asubuhi, maelfu walikuwa wamekusanyika katika Bustani ya Syntagma katikati ya Athens, huku wakisimamiwa na askari wa kuzuia ghasia. Bango moja lilisoma: “Serikali ni wauaji.” Serikali ya mrengo wa kati-kulia ya Waziri Mkuu Kyriakos Mitsotakis ambayo ilishinda tena uchaguzi baada ya ajali ya mwaka 2023, imekabiliwa na ukosoaji mara tena kutoka kwa ndugu wa wahanga kwa kushindwa kuanzisha uchunguzi wa bunge ikiwa ni kuwajibika kisiasa. Serikali imekanusha kufanya makosa yoyote na kusema ni juu ya mahakama kuchunguza ajali hiyo. - Reuters #athens #ugiriki #ajali #treni #mahakama #mgomo #wafanyakazi #ndege #majini #treni
Maelfu ya watu wakusanyika miji mbalimbali kushinikiza haki ifanyike
- 26 Jun 2025 - Some 26 Nyandarua County government vehicles were torched during Wednesday’s demonstrations to mark the first anniversary of last year’s anti-Finance Bill protests.
- 26 Jun 2025 - Iran's intelligence services have arrested 26 people, accusing them of collaborating with Israel, state media Fars news agency reported, days after a ceasefire between the two countries was announced.
- 26 Jun 2025 - Sixteen people died during nationwide anti-government protests in Kenya on Wednesday, most of them killed by police, the head of Amnesty Kenya said, a year after deadly demonstrations against a tax bill culminated in the storming of parliament.
- 26 Jun 2025 - Ecuador's president announced Wednesday that the country's most-wanted fugitive, Los Choneros gang leader "Fito," had been recaptured over a year after his escape from prison triggered a wave of violence.
- 26 Jun 2025 - In a statement on X, Kaluma said the CA’s move was in the interest of public safety and order.
- 26 Jun 2025 - Israeli attacks across Gaza on Wednesday killed at least 45 Palestinians, including some who were seeking aid.
- 26 Jun 2025 - The Triple Olympic champion Faith Kipyegon is on the brink of making history again as she gears up for a landmark sub-four-minute mile attempt at the Charlety Stadium in Paris on Thursday, June 26, 2025, evening. With a Ksh13 million incentive on the…
- 26 Jun 2025 - The communications authority of Kenya has defied court orders barring the action.
- 26 Jun 2025 - Prime Cabinet Secretary and Cabinet Secretary for Foreign and Diaspora Affairs, Musalia Mudavadi, hosted and bid farewell to the United States Chargé d’Affaires, Marc Dillard, as he concludes his diplomatic mission in Kenya. During their meeting,…
- 26 Jun 2025 - Lusaka challenged public officials to internalise and uphold Chapter Six of the constitution in their daily operations.